• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

MKUU WA MKOA WA NJOMBE ATOA WITO KUHUSU USIMAMIZI WA ZAO LA PARACHICHI

Posted on: September 25th, 2025


Njombe, Septemba 25, 2025 – Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, ametoa wito kwa Wakurugenzi wa Halmashauri pamoja na Wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanaweka utaratibu mzuri wa ukusanyaji wa mapato kupitia zao la parachichi, ambalo limeendelea kuwa mkombozi mkubwa wa kiuchumi kwa wakulima wa mkoa huo.

Akizungumza hayo Septemba 25,2025 katika mkutano wa wadau wa kilimo ulioandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) kwa kushirikiana na Taasisi ya TAHA, Mhe. Mtaka alisisitiza umuhimu wa kuweka mifumo rafiki ya ukusanyaji wa ushuru inayolinda maslahi ya mkulima.

“Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi tengenezeni utaratibu mzuri wa kushughulikia zao la parachichi hasa linapofika getini, Muwe na mfumo wa ukusanyaji wa ushuru usiowakandamiza wakulima bali uwe rafiki na unaolinda thamani ya zao hili muhimu,” alisema Mhe. Mtaka.

Mkutano huo uliofanyika kwa lengo la kuzindua rasmi msimu wa ununuzi wa parachichi mwaka 2025, ambapo uliwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo wakiwemo wakulima, wanunuzi, wasafirishaji na wawakilishi kutoka taasisi mbalimbali za maendeleo ya kilimo.

Mhe. Mtaka aliwataka viongozi hao wa halmashauri kuwa wabunifu katika kuanzisha vyanzo vya mapato ambavyo haviwaumizi wakulima bali vinaongeza tija na ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya halmashauri.

“Niombe Wakurugenzi wa Halmashauri kuja na mbinu bunifu za kuongeza mapato bila kumuumiza mkulima. Parachichi ni lulu ya Njombe – tusiiuze kwa hasara kwa sababu ya kukosekana kwa utaratibu mzuri,” aliongeza.

Zao la parachichi limekuwa likipata umaarufu mkubwa kwa  ndani na nje ya nchi kutokana na ubora wake, na linatajwa kuwa moja ya mazao ya kimkakati ya biashara kwa mkoa wa Njombe. Kupitia mashirikiano ya wadau mbalimbali, wakulima wameweza kupata masoko ya kimataifa na kuongeza kipato cha kaya.

Mkutano huo ulihitimishwa kwa maazimio ya pamoja kutoka kwa wadau, likiwemo azimio la kuimarisha ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi katika kuendeleza mnyororo wa thamani wa zao la parachichi kwa manufaa ya taifa

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MKUU WA MKOA WA NJOMBE AKUTANA NA TANESCO NA WAZALISHAJI WADOGO MKOANI NJOMBE

    September 26, 2025
  • MKUU WA MKOA WA NJOMBE ATOA WITO KUHUSU USIMAMIZI WA ZAO LA PARACHICHI

    September 25, 2025
  • WANANCHI NJOMBE KUNUFAIKA NA HUDUMA ZA MADAKTARI BINGWA36

    September 21, 2025
  • Mh.ANTHONY MTAKA AKUTANA NA VIONGOZI WA DL GROUP NA WAFANYABIASHARA WA MKOA WA NJOMBE

    September 18, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.