• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

WAZIRI MASAUNI AFANYA ZIARA YA UKAGUZI KATIKA MRADI WA JESHI LA ZIMAMOTO MKOANI NJOMBE

Posted on: September 30th, 2024

Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Hamad Y. Masauni, amefanya ziara katika mkoa wa Njombe ambapo alikagua maendeleo ya miradi ya ujenzi wa miundombinu ya kikosi cha Zimamoto na Polisi. Katika ziara hiyo, Waziri Masauni alitembelea mradi wa ujenzi wa Ofisi na Kituo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linaloendelea kujengwa mjini Njombe, mradi ambao uko katika hatua za mwisho za kukamilika. Akiwa katika eneo hilo, alieleza kuridhishwa kwake na kasi ya ujenzi, huku akisistiza umuhimu wa kuwa na miundombinu imara kwa ajili ya kuimarisha huduma za zimamoto mkoani humo.

Aidha, Mhe. Masauni alitembelea jengo la polisi la mkoa wa Njombe ambalo limekamilika hivi karibuni. Jengo hilo jipya limejengwa kwa lengo la kuboresha mazingira ya kazi kwa askari wa polisi pamoja na kuboresha huduma kwa wananchi wa Njombe. Alisisitiza kuwa serikali itaendelea kuwekeza katika miundombinu ya usalama ili kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi na kuongeza ufanisi wa vikosi vya usalama.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Zimamoto wa Mkoa wa Njombe, Mrakibu Msaidizi Joel B. Mwakanyasa, mradi wa jengo la ofisi za Zimamoto unatarajiwa kukamilika kwa gharama ya shilingi milioni 700, ambapo tayari asilimia kubwa ya vifaa na rasilimali zimeshatumika. Mradi huo unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi michache ijayo. Waziri alitoa wito kwa wahandisi kuhakikisha kuwa wanakamilisha mradi huo kwa ubora unaostahili na ndani ya muda uliopangwa.

Vilevile, jengo la polisi limekamilika kwa gharama ya shilingi bilioni 1.4, na limejengwa kwa viwango vya juu ili kuhakikisha linaendana na mahitaji ya kisasa ya kikosi cha polisi. Waziri alihitimisha ziara yake kwa kuwapongeza wadau wote walioshiriki katika ujenzi wa miradi hiyo muhimu, na akaahidi ushirikiano wa serikali katika kuhakikisha kuwa miradi mingine ya usalama inatekelezwa mkoani Njombe.

Ziara hiyo iliendeshwa chini ya uongozi wa Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, aliyeiwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Mhe. Kissa Gwakisa, akishirikiana na Katibu Tawala wa Mkoa, Bi. Judica Omari, pamoja na Kamati ya Usalama ya Mkoa.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASILI MKOANI NJOMBE KWA SHANGWE.

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA MTAKA AWAPONGEZA NA KUWAPA HAMASA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA MKOANI NJOMBE.

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA YA UONGOZI YA TASAF AMEANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI NJOMBE.

    April 28, 2025
  • HERI YA SIKU YA MUUNGANO.

    April 26, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.