• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

ONE VOICE ORGANIZATION NJOMBE WAUNGANA NA SERIKALI KUTOA ELIMU YA UKATILI WA KIJINSIA KWA WAZAZI NA WALEZI MTAA WA LUNYANYWI

Posted on: December 16th, 2024

Shirika lisilo la kiserikali la One Voice Organization kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe, limeendesha kampeni ya kutoa elimu ya ukatili wa kijinsia kwa wazazi na walezi. Lengo kuu la kampeni hiyo ni kuwahimiza wazazi kuwalinda watoto wao dhidi ya ukatili wa kijinsia, hususan katika msimu wa sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya.

Elimu hiyo ilitolewa Desemba 16, 2024, katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Ofisi ya Mtaa wa Lunyanywi. Akizungumza katika mkutano huo, Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Mji Njombe, Vickiana Kiwelu, aliwataka wazazi kuwa waangalifu zaidi wakati wa kipindi cha sikukuu kwa kuhakikisha watoto wanakuwa salama.

"Katika kipindi hiki cha sikukuu, tunapaswa kuwa waangalifu sana kuhusu watoto wetu, hasa tunapopokea wageni nyumbani. Si kila mgeni ana nia njema. Kama unajua nyumba yako ni ndogo na unalazimika kupokea mgeni, mtafutie malazi sehemu nyingine ili kumlinda mtoto dhidi ya vitendo vya ukatili. Tuchukue tahadhari kwa sababu baadhi ya ndugu huja na nia ovu," alisema Kiwelu.

Kwa upande wake, Afisa Miradi wa One Voice Organization, Bw. Paul Kapinga, aliwahimiza wananchi kuwa mabalozi wa kuzuia vitendo vya ukatili wa kijinsia. Aliwataka kuhakikisha wanazingatia utu na kutojichukulia sheria mkononi pale wanapokutana na changamoto za kijamii.

"Tuwe mabalozi wa kuzuia ukatili wa kijinsia, hususan kwa watoto. Pale mambo magumu yanapojitokeza, ni muhimu kuzingatia utu na taratibu za kisheria badala ya kujichukulia sheria mkononi," alisema Kapinga.

Aidha, Kiwelu aliwataka wazazi wanaoishi katika ndoa zilizovunjika au kutengana kuhakikisha wanatekeleza jukumu lao la kuwahudumia watoto, akibainisha kuwa kumekuwepo na ongezeko la kina mama kufurika kwenye ofisi za serikali kudai matunzo ya watoto wakati ni jukumu la pamoja la wazazi wote wawili.

"Naomba wazazi, hasa wale walio katika ndoa zilizovunjika, wajitahidi kutimiza jukumu la malezi ya watoto wao. Tumeona ongezeko kubwa la kina mama kufika ofisi za serikali kudai matunzo ya watoto, jambo ambalo linaweza kuepukwa kama wazazi watazingatia majukumu yao," alisisitiza Kiwelu.

Elimu hii inalenga kuhakikisha watoto wanakuwa salama wakati wa sikukuu na kuimarisha mshikamano wa familia katika kupinga ukatili wa kijinsia.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASILI MKOANI NJOMBE KWA SHANGWE.

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA MTAKA AWAPONGEZA NA KUWAPA HAMASA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA MKOANI NJOMBE.

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA YA UONGOZI YA TASAF AMEANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI NJOMBE.

    April 28, 2025
  • HERI YA SIKU YA MUUNGANO.

    April 26, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.