• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

KATIBU TAWALA MKOA WA NJOMBE BI. JUDICA OMARI AFUNGUA MAFUNZO ELEKEZI KWA WATUMISHI WAPYA

Posted on: August 20th, 2025

Mafunzo elekezi kwa watumishi wapya wa umma yanaendelea katika Ukumbi wa Mikutano wa Idara ya Afya Njombe, yakihusisha jumla ya watumishi 47 waliopokelewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa katika mwaka wa fedha 2024/25.

Mafunzo hayo yamefunguliwa rasmi na Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe, Bi. Judica Omari, ambaye amewataka watumishi wapya kutumia fursa hiyo kujifunza na kuzingatia kanuni za utumishi wa umma kwa ajili ya kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Bi. Omari alisema: “Ninawasihi mtumie nafasi hii kujifunza kwa makini, mzingatie maadili ya kazi na kuwa waadilifu katika kila mtendaji. Serikali imewaamini na kuwapa nafasi hii, hivyo ni wajibu wenu kuhudumia wananchi kwa weledi na uaminifu.”

Katika mafunzo hayo, mada mbalimbali zinafundishwa na wataalamu kutoka ofisi na taasisi za Serikali. Mada hizo ni pamoja na: Muundo na Majukumu ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa, Kanuni za Maadili ya Utendaji katika Utumishi wa Umma, Wajibu, Haki, Makosa na Adhabu katika Utumishi wa Umma, Elimu ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Elimu ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (PSSSF), pamoja na Wajibu wa Vyama vya Wafanyakazi mahali pa kazi. Vilevile washiriki wanapatiwa elimu kuhusu Lishe na VVU/UKIMWI, Mifumo tumizi ya TEHAMA Serikalini, na Mfumo wa Usimamizi na Upimaji wa Utendaji Kazi kwa Watumishi (Watumishi Portal).

Mafunzo haya ni utekelezaji wa Kanuni G.1(8) ya Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma za mwaka 2009, inayomtaka Mwajiri kuandaa mafunzo elekezi kwa watumishi wapya wanaoingia Serikalini ili wawe na uelewa wa taratibu, maadili na miiko ya kazi za umma. Kupitia mafunzo hayo, washiriki wanatarajiwa kufahamu dira, dhima na malengo ya taasisi, kujengewa uelewa wa haki na wajibu wao, kutambulishwa majukumu na viwango vya utekelezaji kazi, pamoja na kupewa mbinu za kukabiliana na changamoto za kikazi na kijamii.

Kupokelewa kwa watumishi wapya 47 mkoani Njombe kumeondoa pengo la upungufu wa watumishi lililokuwepo katika Sekretarieti ya Mkoa na Ofisi za Wakuu wa Wilaya, hatua ambayo inatarajiwa kuongeza ufanisi na kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • KATIBU WA CHAMA CHA WAFANYAKAZI TUGHE MKOA WA NJOMBE AWASISITIZA WATUMISHI WAPYA KUJIUNGA NA VYAMA VYA WAFANYAKAZI.

    August 20, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA NJOMBE BI. JUDICA OMARI AFUNGUA MAFUNZO ELEKEZI KWA WATUMISHI WAPYA

    August 20, 2025
  • IFAD YATAMBULISHA MRADI WA MAZIWA MKOANI NJOMBE.

    August 19, 2025
  • NJOMBE: WAKUU WA IDARA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA MANUNUZI YA UMMA.

    August 18, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.