• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

MKUU WA MKOA AZUNGUMZA NA WAFANYABIASHARA WA MBAO KUHUSIANA NA VIBALI

Posted on: September 22nd, 2023

Zaidi ya malori mia mbili ya mazao ya misitu mkoani Njombe yamekwama kutokana na kukwama kwa mfumo wa malipo ya tozo za vibali vya usafirishaji wa mazao ya misitu kwa zaidi ya wiki moja.

Wakizungumza mbele ya mkuu wa mkoa wa Njombe Anthony Mtaka leo wafanyabiashara hao walisema Julai mwaka huu kuelekea mwaka mwingine wa fedha malori hayo.yalikwama kusafirisha mbao kwa muda wa wiki moja na baadae kuruhusiwa baada ya kutolewa kwa malalamiko na wafanyabiashara hao.

Walisema licha ya kukatiwa ushuru lakini baada ya kufuatilia kibali cha kusafirisha mbao kinachotolewa na Wakala wa Misitu mkoani Njombe wakaambiwa mfumo unasumbua hivyo kusababisha kupaki malori kwa muda mrefu licha ya kuwa na mzigo.

Walisema na safari hii jambo hilo limejirudia tena ambapo zaidi ya wiki sasa malori ya kusafirisha mbao yamekwama kutokana na kile kinachodaiwa kukwama kwa mfumo wa vibali vya kusafirisha misitu.

Walisema biashara wanayoifanya inategemea mikopo kutoka taasisi za fedha hivyo wanavyoendelea kusubiri mfumo ukae sawa marejesho yanahitajika hivyo wanapata wakati mgumu.

Walisema kukwama kwa malori hayo kwa muda mrefu kuna sababisha kupungua kwa uaminifu kwa wateja wao ambao wamekuwa wakifanya biashara nao kutokana kuchelewesha bidhaa zao.

Baadhi ya wafanyabiashara hao wakiwemo Sophia Raymond na Subira Kyando waliiomba serikali kupunguza vituo vya ukaguzi wa mazao ya misitu kwani vimekuwa vikileta usumbufu kwa kuchukua muda mrefu wa safari.

"Hii faini ambayo maliasili yamekuwa wakiwapiga madereva sababu ya kuruka kituo bila kukaguliwa ni uonevu kwasababu madereva wengine ni wageni hivyo kuwe na vituo vichache vitakavyotambulika kwa urahisi" alisema Raymond.

Wakala wa Misitu mkoa wa Njombe Audatus Kashamakula alikiri kuwepo kwa changamoto hiyo na kudai kuwa imetokana na kusimama kwa mifumo ya utozaji kodi ya Wizara ya Fedha jambo ambalo lipo nje ya uwezo wao kwasasa.

Alisema wamekuwa wakijitahidi kutoa huduma hata muda wa ziada ili kupunguza changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza katika utoaji wa vibali.

"Nipende kuwaomba radhi wadau wetu wa mazao ya misitu wasafirishaji na madereva kwa hili ambalo limetokea na tutafanyia kazi changamoto zote ambazo zimetokea hasa mfumo ambao ulikuwa haujakaa sawa" alisema Kashamakula.

Mkuu wa mkoa wa Njombe Anthony Mtaka aliziomba wizara zinazohusika kushughulikia tatizo hilo haraka ili kunusuru mapato ya mkoa huo ambayo zaidi ya asilimia sabini yanategemea mazao ya misitu.

Alisema uchumi wa mkoa wa Njombe zaidi ya asilimia sabini unategemea mazao yatokanayo na misitu hivyo lazima kuwepo na usimamizi utakaoweka mazingira mazuri ya wafanyabiashara wa mazao ya misitu.

"Mbao inabeba zaidi ya asilimia sitini hadi sabini ya uchumi wa mkoa hivyo tunao wajibu wa kuhakikisha tunaweka mazingira mazuri ya biashara kuliko kuwaza kukusanya tu" alisema Mtaka

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • PROF. MUKANDALA AONGOZA VIONGOZI KUSHUHUDIA UTIAJI SAINI WA MKATABA WA UJENZI WA KAMPASI YA UDOM MKOANI NJOMBE.

    May 17, 2025
  • MPANGO WA NJOMBE KUPUNGUZA UDUMAVU WAZINDULIWA RASMI.

    May 17, 2025
  • KAMATI YA USALAMA YA MKOA WA NJOMBE YAMPA POLE KAMISHNA MWANDAMIZI WA UHAMIAJI FELISTA SANGA KUFUATIA MSIBA WA MUMEWE.

    May 17, 2025
  • MKUU WA MKOA WA NJOMBE MHE. ANTHONY MTAKA AKUTANA NA MKURUGENZI WA KAMPUNI YA KANJI LALJI, AMKARIBISHA KUWEKEZA MKOANI NJOMBE KATIKA KILIMO CHA KAHAWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.