• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA LUDEWA AKUTANA NA VIONGOZI WA DINI NA KISIASA KUJADILI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA.

Posted on: September 27th, 2024


Na. Chrispin Kalinga - Ludewa, Njombe

Ludewa, Njombe – Septemba 26, 2024 – Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa, Ndugu Sunday Deogratias, jana alifanya mkutano muhimu na viongozi wa dini pamoja na viongozi wa vyama vya siasa kujadili maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwezi Novemba mwaka huu.

Akizungumza katika mkutano huo, Ndugu Deogratias alisisitiza umuhimu wa viongozi wa dini na siasa kushirikiana kwa karibu ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani, uwazi, na haki. Alieleza kuwa mchango wa viongozi hao katika kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu ni wa msingi kwa maendeleo ya demokrasia na ustawi wa jamii katika wilaya ya Ludewa.

“NINAWAOMBA VIONGOZI WA DINI NA VYAMA VYA SIASA KUWAHAMASISHA WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI KATIKA MCHAKATO WA UCHAGUZI, KICHUKUE FOMU NA KUGOMBEA NAFASI ZA UONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA. UCHAGUZI HUU NI FURSA YA KUJENGA SERIKALI ZA KIUWAJIBIKAJI NA ZENYE KUZINGATIA MAENDELEO YA WANANCHI,” alisema Deogratias.

Pia, Ndugu Deogratias alieleza kuwa serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa njia ya haki, huku akisisitiza kuwa vyama vya siasa vina wajibu wa kuepuka vurugu na maneno ya uchochezi. Aliongeza kuwa ni muhimu kila mgombea na chama kuzingatia taratibu na kanuni zilizowekwa ili kulinda amani wakati wa uchaguzi.

Kwa upande wa viongozi wa dini, waliombwa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha jamii zinaendelea kuwa na utulivu, hususan katika kipindi hiki cha kampeni na uchaguzi. “VIONGOZI WA DINI MNA NAFASI YA KIPEKEE KATIKA KUWAONGOZA WANANCHI KUSIMAMA KATIKA ZILIZO SAHIHI, KUWEKA MBELE AMANI NA MAENDELEO YA JAMII YETU,” aliongeza.

Mkutano huo ulihudhuriwa na wawakilishi kutoka madhehebu mbalimbali pamoja na viongozi wa vyama vya siasa ambao walitoa michango yao kuhusu namna bora ya kuhakikisha uchaguzi wa Serikali za Mitaa unafanikiwa na kutoa viongozi watakaowajibika kwa wananchi.

Mwisho, Ndugu Deogratias aliwataka wananchi wa Ludewa kushiriki kwa wingi katika mchakato wa uchaguzi kwa kujiandikisha, kuchukua fomu za kugombea, na kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura ili sauti yao isikike na kuchangia maendeleo ya jamii.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASILI MKOANI NJOMBE KWA SHANGWE.

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA MTAKA AWAPONGEZA NA KUWAPA HAMASA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA MKOANI NJOMBE.

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA YA UONGOZI YA TASAF AMEANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI NJOMBE.

    April 28, 2025
  • HERI YA SIKU YA MUUNGANO.

    April 26, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.