Mafunzo hayo yameandaliwa na Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) mkoa wa Njombe, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa serikali kuhakikisha madereva wake wanazingatia sheria, taratibu na miongozo ya usalama barabarani sambamba na kudumisha maadili ya kazi.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, mmoja wa wakufunzi kutoka TEMESA Mhandisi Charles Mbogolo ambaye ni Meneja Ufundi na Matengenezo, amesema kuwa mafunzo haya ni ya muhimu kwani mbali na kuongeza ufanisi, pia yanasaidia kuimarisha usalama wa abiria, watumiaji wa barabara na vyombo vya usafiri vinavyomilikiwa na serikali.
"Mafunzo haya si ya kawaida. Ni mwendelezo wa juhudi za serikali kupitia TEMESA kuhakikisha kuwa kila dereva wa serikali anakuwa na uelewa mpana kuhusu sheria za usalama barabarani, namna ya kujilinda dhidi ya majanga kama moto, na pia kuwa na uelewa juu ya masuala muhimu ya kitaifa kama uhamiaji haramu na vita dhidi ya rushwa," alieleza.
Miongoni mwa mada zilizowasilishwa kwa madereva hao ni pamoja na:
Tahadhari dhidi ya moto kwenye magari na majengo,
Uhamiaji haramu na namna ya kushiriki katika udhibiti wake,
Rushwa na madhara yake katika utumishi wa umma,
Usalama barabarani na uzingatiaji wa sheria.
Madereva walioshiriki wameeleza kufurahishwa na mafunzo hayo wakisema yamekuja wakati muafaka, hasa kwa kuzingatia changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo katika kazi zao za kila siku.
Mtaa wa Lunyanywi
Postal Address: P.O.Box 668-Njombe
Telephone: 026 278 291 213
Mobile:
Email: ras@njombe.go.tz
Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.