• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

KAMPUNI YA ITRACOM YAZINDUA GHALA LA KUHIFADHIA MBOLEA MKOANI NJOMBE

Posted on: November 11th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Anthony Mtaka ametoa rai kwa wafanyakazi wa makampuni na wazalishaji wa mbolea nchini kuepuka udanganyifu na uchakachuaji wa mbolea hali inayoumiza wakulima na kutia hasara Taifa.

Mtaka ameyasema hayo mara baada ya kuzindua ghala la kuhifadhia mbolea za kampuni ya ITRACOM ya Mkoani hapa,alisema msimu wa kilimo iliyoisha kumefanyika sana vitendo vya udanganyifu.

‘’Kampuni moja sitaki kuitaja jina kwa sababu ya biashara hapa Njombe,msimamizi wa ghala alifanya mchezo kwenye akawa anapaki mbolea aina hiyo anaweka mchanga,mteja anajua ni mbolea imefungwa kumbe ni mchanga, lakini tulipata wasimamizi wa magodaun wanafanya michezo na wafanyabiashara ambao sio waaminifu’’alisema.

Mtaka alisema‘’mfuko umepimwa kilo 25 unapunguzwa kilo nne inabaki 21,mfuko ni kilo 50 anatoa tano inabaki 45,anachukua mchanga mweupe,anasaga chumvi anachanganya hadi mchele kwenye mbolea’’

Mtaka ametoa wito kwa wasimamizi wa maghala kuwa waaminifu na kuacha michezo michafu kwa sababu ya kuchukua mchanga na kwenda kuweka kwenye maghala ili kuonekana kwamba mbolea ipo nyingi.

Hata hivyo Mtaka ameongeza kuwa mahitaji ya mbolea kwa sasa mkoa wa Njombe ni tani 112,000 na kutoa wito kwa wafanyabiashara kuchangamkia fursa ya kuwekeza ili wakulima wasikose mbolea.

Mawakala wadogo wa pembejeo mkoa wa Njombe akiwemo Olaph Mhema waliomba mbolea zinazozalishwa nchini zipunguzwe bei na kusambazwa kwa wakati.

‘’Mbolea za Intracom bado zipo bei kubwa sana,wanazalisha kilo 25 hawana kilo 50 lakini bado inagharama kubwa sana kwa hiyo haiwezi kushindana na mbolea za nje,kiwanda ni cha kwetu kama wanakwama kwenye uzalishaji serikali muingilie kati’’alisema.

Nae Mkurugenzi wa Biashara na Masoko Itracom Dk. Keneth Masuki alisema mbolea hiyo tayari imeshambazwa zaidi ya mikoa Kumi  na Nane ambapo kwa msimu uliopita mbolea aina Tatu zimezalishwa zikiwemo Fomi otesha, Fomi kuzia na Fomi nenepesha.

‘’Mkakati wa usambazaji wa mbolea zetu kwa msimu uliopita tulifika mikoa karibu 18,sasa hivi tumeona tufungue maghala baadhi kwa kuanzia ili mbolea iwe karibu na wateja wadogo wadogo,mawakala ambao hawawezi kuchukua lori zima’’alisema Masuki.




Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASILI MKOANI NJOMBE KWA SHANGWE.

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA MTAKA AWAPONGEZA NA KUWAPA HAMASA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA MKOANI NJOMBE.

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA YA UONGOZI YA TASAF AMEANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI NJOMBE.

    April 28, 2025
  • HERI YA SIKU YA MUUNGANO.

    April 26, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.