• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

WAZIRI MKUU MAJALIWA AMALIZA ZIARA YAKE WILAYA YA WANGING’OMBE.

Posted on: March 22nd, 2025

Njombe, 22 Machi 2025 – Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, amehitimisha ziara yake katika Wilaya ya Wanging’ombe baada ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo, pamoja na kuhutubia wananchi katika mikutano ya hadhara iliyofanyika kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi Ilovi-Makoga na baadaye katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Igwachanya.


Akiwahutubia wananchi katika Viwanja vya Shule ya Msingi Ilovi-Makoga, Mhe. Majaliwa aliipongeza Wilaya ya Wanging’ombe kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita. Aliwahimiza wananchi kushiriki kikamilifu katika ulinzi wa miradi hiyo ili kuhakikisha inawanufaisha kwa muda mrefu. Aidha, aliwakumbusha wazazi na walezi umuhimu wa kuhakikisha watoto wanapata elimu, akisisitiza kuwa hilo si hiari bali ni wajibu wa kila mzazi.


Baada ya mkutano huo, Waziri Mkuu alikagua ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka Itulahumba hadi Igwachanya yenye urefu wa kilomita 19.25. Ujenzi wa barabara hiyo umefikia asilimia 86 na unatarajiwa kukamilika kwa gharama ya shilingi bilioni 9.8. Mhe. Majaliwa alisisitiza kuwa serikali itaendelea kuwekeza katika miundombinu ya barabara ili kuboresha usafiri na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika Mkoa wa Njombe.


Ziara hiyo ilihitimishwa kwa mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Igwachanya, ambapo Waziri Mkuu alizungumzia uwekezaji mkubwa unaofanywa na serikali katika sekta ya elimu. Akitolea mfano Shule ya Sekondari ya Mkoa ya Wasichana ya Njombe, iliyojengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 4, Mhe. Majaliwa aliwataka wanafunzi wote kuzingatia masomo na kuonesha mshikamano kwa wenzao wenye mahitaji maalum. Katika hotuba yake ya kumaliza ziara, alimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, kwa usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo mkoani humo, akibainisha kuwa juhudi hizo zinaakisi dhamira ya serikali ya kuwaletea wananchi maendeleo endelevu.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASILI MKOANI NJOMBE KWA SHANGWE.

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA MTAKA AWAPONGEZA NA KUWAPA HAMASA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA MKOANI NJOMBE.

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA YA UONGOZI YA TASAF AMEANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI NJOMBE.

    April 28, 2025
  • HERI YA SIKU YA MUUNGANO.

    April 26, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.