• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

WAZIRI MKUU MAJALIWA AMALIZA ZIARA YA SIKU TATU MKOANI NJOMBE.

Posted on: March 20th, 2025

Njombe, 23 Machi 2025 – Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, leo amehitimisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe, ambapo amekagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuzungumza na wananchi kuhusu juhudi za serikali katika kukuza uchumi wa viwanda.


Akiwa katika siku yake ya mwisho ya ziara, Mhe. Majaliwa alihutubia wananchi wa Makambako kwenye mkutano wa hadhara, akiwahimiza kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na kuitumia fursa ya kilimo cha parachichi kuinua uchumi wao.


Baada ya mkutano huo, alitembelea Kiwanda cha Kusindika Parachichi cha AVOAFRICA, kilichopo katika Halmashauri ya Mji wa Makambako, ambacho kinaendelea kuongeza thamani ya zao la parachichi kwa ajili ya soko la ndani na la kimataifa. Katika ziara hiyo, alisifu juhudi za wawekezaji na kuhimiza uendelezaji wa viwanda vya kusindika mazao mengine ya kilimo.


Aidha, Mhe. Majaliwa alitembelea Kiwanda cha Kuchuja Mafuta ya Parachichi kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Wanging’ombe, ambapo alieleza kuwa uwekezaji huo ni hatua muhimu katika kuongeza thamani ya mazao ya wakulima na kuongeza fursa za ajira kwa vijana wa Njombe.


Katika hotuba yake, Waziri Mkuu alimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, kwa jitihada kubwa za kupanua wigo wa uchumi wa viwanda mkoani humo.


"Njombe inakuwa mfano mzuri wa uchumi wa viwanda. Tayari tunaona Kiwanda cha Kusindika Parachichi kinafanya kazi, Kiwanda cha Kuchuja Mafuta ya Parachichi nacho kinaendelea na uzalishaji, na bado kuna viwanda vingine vinajengwa hapa hapa Njombe. Tunashuhudia pia ujenzi wa Kiwanda cha Kuchakata Chuma na Kuunda Magari. Hili ni jambo la kupongeza sana. Hongera sana Mkuu wa Mkoa kwa kazi nzuri ya kuvutia uwekezaji na kufanikisha mapinduzi ya viwanda hapa Njombe,” alisema Mhe. Majaliwa.


Ziara ya Waziri Mkuu mkoani Njombe ilikuwa na lengo la kukagua miradi ya maendeleo, kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika uchumi wa viwanda, na kuhakikisha rasilimali za mkoa zinatumika ipasavyo kwa manufaa ya wananchi wote.


Mwisho.



Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASILI MKOANI NJOMBE KWA SHANGWE.

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA MTAKA AWAPONGEZA NA KUWAPA HAMASA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA MKOANI NJOMBE.

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA YA UONGOZI YA TASAF AMEANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI NJOMBE.

    April 28, 2025
  • HERI YA SIKU YA MUUNGANO.

    April 26, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.