• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

SERIKALI KUNUNUA NGANO ITAKAYOPATIKANA MAKETE

Posted on: June 30th, 2023

Serikali imewahakikishia wakulima wilayani Makete mkoani Njombe kuwa itanunua ngano yote inayozalishwa sambamba na kuifanya wilaya hiyo kuwa kitovu cha uzalishaji wa zao hilo.Ahadi hiyo imetolewa na waziri wa kilimo Hussein Bashe,wakati akizungumza kwa njia ya simu katika mkutano cha maandalizi ya msimu wa kilimo cha ngano mwaka 2023/24 wilayani Makete,alisema kilo moja itanunuliwa kwa shilingi 1000 na si vyenginevyo.

"Ni shilingi 1000 ndiyo bei atakayonunua CPB(bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko)na ngano iliyopo sasa hivi itakayovunwa mwaka huu pia watanunua"alisema Bashe. Aliongeza kuwa"Makete tutaifanya kama wilaya ya majaribio mwaka huu watalima tani 1000 kwa kuwa mahesabu yanaendelea,tutaifunga wilaya ya Makete baada ya soil analysis report(ripoti ya uchambuzi wa udongo) kukamilika kuwa ni production area(eneo la uzalishaji)ya ngano peke yake,najua mtaniuliza mahindi tutakula wapi,tutakapoifunga tutatafuta solution iko wapi,tutajua mahindi tunakula wapi’’alisema Bashe.Aidha Bashe alisema pindi zoezi la urasimishaji ardhi litakapokamilika wakulima watakuwa na fursa ya kumiliki ardhi.

 Katibu mkuu wizara ya ardhi Antony Sanga,alisema kuwa kupitia mpango wa matumizi ya ardhi Rais Samia Suluhu Hassan ametoa kiasi cha shilingi milioni 378 kwa ajili ya zoezi hilo.

"Kwa hapa Makete kwa awamu hii tumepata vijiji 44 kati ya 4,131 nchi nzima ambavyo vinaandaliwa mapango wa matumizi ya ardhi,mpango wa matumizi ya ardhi tunapoutekeleza na kukamilisha tafrili yake tunakwenda kupanga maeneo vizuri ya makazi lakini maeneo ya kilimo,maeneo ya malisho,maeneo ya uwekezaji,maeneo rasmi ya vyanzo vya maji,hifadhi za misitu lakini pia kutatua migogoro ambapo migogoro 16 imetatuliwa hapa Makete’’alisema Sanga.

Mkuu wa mkoa wa Njombe Antony Mtaka alimueleza waziri Bashe changamoto ya kukosekana kwa maghala ambayo yatarahisishia wakulima kuhifadhi mazao yao.Mtaka alisema kuwa hakuna sababu ya kuwafanya wananchi ya Makete kushindwa kulima ngano badala yake wanapaswa kuweka maamuzi."Tutoke kwenye watu wa kuzoea kukusanya kukusanya tu,tumewekeza nini?’’alihoji Mtaka. Mtaka amesema Mkakati wa zao la Ngano kuzalishwa kwa wingi Wilayani Makete ni matunda ya Watumishi ambao wameanza kushirikiana na wananchi kwenye Kilimo, mikopo na utoaji wa elimu.

“Niwapongeze watumishi Halmashauri ya Wilaya ya Makete na huu ni mfano wa kuigwa na Halmashauri zingine ndani ya Mkoa wa Njombe na ndio maana nimewaita Wakurugenzi wote wa Halmashauri, Wenyeviti wote na Wakuu wa Wilaya zote mjifunze kitu kinachofanywa Makete”.

Mkurugenzi wa uzalishaji kutoka wakala wa mbegu za kilimo ASA Jastine Ringo,alisema wamesaini mikataba mitatu ya kuchukuwa mbegu wilayani humo.

"Sisi kama wakala tutazichukua zote ambazo zimekidhi kuwa mbegu kwa sababu kuna tofauti ya mbegu na nafaka kwa hiyo wakati wa kuzunguka tumeshaingia mkataba na vikundi viwili vya vijana pamoja na mkulima mmoja,huu ni mwanzo tu msimu unaokuja tunarajia kuchukua ngano nyingi zaidi,tutaingia mkataba na wakulima wengi zaidi ninaona maono makubwa kwa wilaya ya

Makete,ninaona kiwanda kikubwa pamoja na shamba kubwa la mbegu ambalo mtakuwa mnauzia hapa hapa’’alisema Ringo.

Kaimu mkurugenzi wa bodi ya nafaka na mazao mchanganyiko CPB John Maige alisema kuwa bodi ya nafaka imeanzishwa ili kuhakikisha wakulima wanakuwa na uhakika na mazao wanayozalisha pamoja na kueleza kuwa nchi bado inauhitaji mkubwa wa zao la ngano.Mmoja wa mkazi wa mjini Makete Mexon Sanga,alisema kuwa hapo awali walikuwa wanalima kwa mazoea na hivyo kuiomba serikali kuwezesha kupatikana zana za kisasa za kilimo ili kuweza kuleta tija.

 

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASILI MKOANI NJOMBE KWA SHANGWE.

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA MTAKA AWAPONGEZA NA KUWAPA HAMASA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA MKOANI NJOMBE.

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA YA UONGOZI YA TASAF AMEANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI NJOMBE.

    April 28, 2025
  • HERI YA SIKU YA MUUNGANO.

    April 26, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.