• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

NJOMBE: WAKUU WA IDARA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA MANUNUZI YA UMMA.

Posted on: August 18th, 2025

Njombe –Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu Mkoa wa Njombe, Bw. Lewis Mnyambwa, amewataka Wakuu wa Idara mkoani humo kuzingatia kwa makini sheria za manunuzi ya umma na kuhakikisha tenda zote za serikali zinatangazwa na kushughulikiwa kupitia mfumo wa kielektroniki wa National e-Procurement System of Tanzania (NeST), kama ilivyoelekezwa na mamlaka husika.

Akifungua semina elekezi ya mafunzo ya sheria na matumizi ya mfumo wa ununuzi wa umma (NeST), yanayoratibiwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) kwa siku tano katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Bw. Mnyambwa alisisitiza kuwa kutofuata masharti ya sheria hiyo kutachukuliwa kama uvunjifu wa taratibu na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya yeyote atakayebainika.

“Ni wajibu wa kila kiongozi wa idara kuhakikisha taratibu za manunuzi ya umma zinafuatwa ipasavyo. Mfumo wa NeST umeanzishwa kwa lengo la kuongeza uwazi, kuondoa mianya ya rushwa, na kuhakikisha thamani ya fedha za umma inapatikana. Hivyo hakuna sababu ya mtu yoyote kupuuza maagizo haya,” alisema Bw. Mnyambwa.

Aidha, alifafanua kuwa mfumo wa NeST ni hatua ya kisasa iliyowekwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuhakikisha mchakato wa manunuzi ya umma unakuwa wa haraka, wenye uwazi na unaozingatia ushindani wa haki kwa wazabuni wote.

“Napenda kusisitiza kwamba kuanzia sasa hakuna ununuzi wowote wa serikali utakaofanyika nje ya mfumo wa NeST. Hii ni sheria na maelekezo rasmi ya serikali. Yeyote atakayeenda kinyume na taratibu hizi atawajibishwa kwa mujibu wa sheria,” aliongeza.

Mafunzo hayo ya siku tano yamekusudia kuwajengea uwezo Wakuu wa Idara, Wakuu wa Taasisi, Maafisa Ugavi, na wataalamu wengine kutoka Halmashauri zote za mkoa wa Njombe juu ya utekelezaji sahihi wa sheria ya manunuzi ya umma pamoja na matumizi ya mfumo wa NeST ili kuimarisha uwajibikaji na ufanisi katika usimamizi wa fedha za umma.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • KATIBU WA CHAMA CHA WAFANYAKAZI TUGHE MKOA WA NJOMBE AWASISITIZA WATUMISHI WAPYA KUJIUNGA NA VYAMA VYA WAFANYAKAZI.

    August 20, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA NJOMBE BI. JUDICA OMARI AFUNGUA MAFUNZO ELEKEZI KWA WATUMISHI WAPYA

    August 20, 2025
  • IFAD YATAMBULISHA MRADI WA MAZIWA MKOANI NJOMBE.

    August 19, 2025
  • NJOMBE: WAKUU WA IDARA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA ZA MANUNUZI YA UMMA.

    August 18, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.