• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

MHE. MTAKA ATOA WITO WA KUSHIRIKI KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KATIKA SIKU YA MWALIMU NYERERE.

Posted on: October 14th, 2024

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe, pamoja na Menejimenti yote kwa ujumla, inaungana na Watanzania wote katika kuadhimisha kumbukizi ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius K. Nyerere. Mwalimu Nyerere, aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Tanzania, ni kielelezo cha uongozi wa busara, utu, usawa, na haki. Leo, tunamkumbuka kwa mchango wake mkubwa katika kujenga misingi imara ya taifa huru na lenye umoja.

Katika maadhimisho haya, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe imeeleza kuwa Nyerere aliwaweka wananchi katikati ya kila jitihada za maendeleo ya taifa. Uongozi wake ulizingatia umuhimu wa wananchi kushiriki kikamilifu katika maamuzi na michakato ya maendeleo. Kupitia sera zake za Ujamaa na Kujitegemea, alihamasisha jamii kufanya kazi kwa bidii, kwa pamoja, ili kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anapata nafasi sawa ya kushiriki katika ustawi wa taifa.

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe tunaamini kwamba Mwalimu Nyerere alianzisha tunu za Umoja na Amani ambazo zimekuwa nguzo muhimu katika maendeleo ya Tanzania hadi sasa. Amani aliyoijenga imewezesha taifa letu kuendelea katika mazingira ya utulivu, huku Umoja ukiendelea kuwa chachu ya mafanikio katika sekta mbalimbali za kiuchumi, kijamii, na kisiasa.


Kwa kuhitimisha, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe tunawaeleza wananjombe na watanzania kwa ujumla kuwa, tunaendelea kuenzi na kudumisha maono ya Mwalimu Nyerere. Katika kumbukizi hii, Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Athony Mtaka anawamehimiza wananchi wote wa Mkoa wa Njombe kuendelea kushikamana na kutetea tunu hizi, ili kizazi cha sasa na kijacho kiendelee kufurahia matunda ya uhuru, maendeleo, na amani aliyoyapigania kwa dhati.


Mhe. Mtaka pia ameongeza, "Kama alivyosisitiza Mwalimu, Serikali za Mitaa ni nguzo muhimu katika maendeleo ya taifa. Ni wakati wa wananchi kuonyesha uzalendo wao kwa kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, ili kuhakikisha tunapata viongozi wenye maono na uwezo wa kusimamia maslahi ya jamii. Tunapoelekea uchaguzi huu, ninawahamasisha wananchi wote wa Njombe kujiandikisha mapema na kushiriki kikamilifu kwenye uchaguzi huu wa kihistoria, ili tuendelee kujenga jamii yenye usawa, haki, na maendeleo."

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASILI MKOANI NJOMBE KWA SHANGWE.

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA MTAKA AWAPONGEZA NA KUWAPA HAMASA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA MKOANI NJOMBE.

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA YA UONGOZI YA TASAF AMEANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI NJOMBE.

    April 28, 2025
  • HERI YA SIKU YA MUUNGANO.

    April 26, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.