• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

KAMATI YA SIASA MKOA WA NJOMBE YAHITIMISHA ZIARA KWA KUFANYA MAJUMUISHO

Posted on: October 11th, 2023

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Njombe Mh. Deo Sanga amewaagiza viongozi mkoani Njombe kuhakikisha wanamaliza miradi yote viporo iliyoanzishwa na wananchi.

Agizo hilo alilitoa katika kikao cha majumuisho ya kamati ya siasa mkoa wa Njombe,alisema wamegundua kuwepo kwa changamoto katika sekta ya elimu hususani ujenzi wa maboma viporo ya madarasa pamoja na sekta ya afya.

"Vituo vya afya na zahanati havijakamilika,hivyo basi serikali kupitia Halmashauri zote zikamilishe kwa haraka maboma hayo ili wananchi waweze kuhudumiwa kiufasaha"alisema Sanga.

Sanga pia alimuagiza mkuu wa mkoa wa Njombe Antony Mtaka kuunda tume ili kuchunguza miradi miwili mabwawa ya samaki Mtwango pamoja na kituo cha afya cha kijiji cha Ikondo katika halmashauri ya wilaya ya Njombe ambayo haijakamilika huku fedha nyingi ikitumika.

Sanga alisema kamati ya siasa mkoa ilitembelea kata 81 kati ya kata 107 z mkoa wa Njombe na miradi 81 yenye thamani ya zaidi ya sh bilioni 43 pamoja na mikutano ya hadhara na kusikiliza kero za wananchi.

Mkuu wa mkoa wa Njombe Antony Mtaka,alisema kila halmashauri ijipange na kujua idadi ya miradi viporo ili kuikamilisha kwa wakati.

"Tujipange kwamba kwa mwaka wa fedha 2023/24 miradi hii inaenda kumalizika kwa sababu inawahusu wananchi ambao walichangia kwenye mapato yao waliuza mbuzi,kuku na vitu vyengine hilo ni la kitaalamu kwa maana ya CMT na Ras,lakini jengine katibu tawala kukutana na wakuu wa taasisi,meneja wa Tarura,meneja wa Ruwasa,meneja wa Tanesco,meneja wa Tanroad kuangalia kero za msingi"alisema Mtaka.

Naye katibu wa siasa na uenezi mkoa wa Njombe Josaya Luoga,alitoa onyo baadhi ya viongozi wa chama cha mapinduzi wa wilaya za mkoa wa Njombe wanajihusisha na vitendo vya kukihujumu chama hicho kwa kuanza kuandaa wagombea wao watakao gombea nafasi mbalimbali ikiwemo udiwani na ubunge katika uchaguzi mkuu wa 2025.

Luoga alisema chama hicho kimebaini uwepo wa viongozi wanaohujumu kazi zinazofanywa na wenyeviti,madiwani na wabunge waliopo madaraka kwa kuwasemea vibaya na kuwanadi watu wao na kuahidi kuwachukulia hatua kali za kinidhamu.

"Viongozi hao ni wale wa umoja wa vijana wa chama hicho UVCCM kutoka wilaya ya Ludewa,Makete na Wanging'ombe,tunawajua tunaomba waache mara moja kwa sababu uchaguzi bado"alisema Luoga.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASILI MKOANI NJOMBE KWA SHANGWE.

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA MTAKA AWAPONGEZA NA KUWAPA HAMASA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA MKOANI NJOMBE.

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA YA UONGOZI YA TASAF AMEANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI NJOMBE.

    April 28, 2025
  • HERI YA SIKU YA MUUNGANO.

    April 26, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.