• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI AMALIZA MGOGORO WA MPAKA BAINA YA MAKETE NA WANGINGOMBE

Posted on: November 22nd, 2023

Vijiji saba ilivyopo katika mgogoro wa mpaka kati ya wilaya za Makete na Wanging'ombe mkoani Njombe,ambavyo vilipimwa wakati wa ugawaji wa wilaya vimeagizwa virudiwe kupimwa upya.

Agizo hilo lilitolewa na waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Jerry Silaa wakati wa ziara yake mkoani hapa alisema kwa sababu mchakato wa upimaji uliotumika hapo awali haukuzingatia tangazo la serikali la upimaji wa mipaka.

Agizo hilo limekuja kufuatia timu ya wapimaji wa ramani kutoka wizara ya ardhi kufika na kufanya tafsiri ya tangazo la serikali lililotumika kuanzishwa kwa wilaya ya Makete na Wanging'ombe.

‘’Mipaka ya vijiji vyote vilivyopimwa irudiwe kupimwa upya kwa kuzingatia matangazo ya mipaka ya wilaya kwa kuwa upimaji wa mwanzo haukuzingatia mipaka ya matangazo ya serikali,’’alisema Silaa.

Pia waziri alisema pendekezo la pili wananchi wa pande zote mbili waheshimu mpaka wa wilaya hizo kulingana na tafsiri ya matangazo ya serikali ya mipaka kama yalivyotafsiriwa na timu ya wataalamu.

Waziri Silaa alisema migogoro ya mipaka isiwaingize viongozi kwenye malumbano ambayo hayasaidii.

‘’Lakini kubwa ni yale maelezo yote hasa lile nililosema la kupima upya vijiji,nikimuandikia taarifa yangu mh makamu wa Rais(Dk.Philip Mpango)naamini litafanyika kwa haraka kwa sababu tunaenda kwenye mwaka wa uchaguzi wa vijiji na vitongoji na mitaa kwa hiyo kila mtu ajitambue kuwa yuko wapi,’’alisema Silaa.

Awali wawakilishi wa wananchi kutoka katika vijiji vya kata ya Moronga wilaya ya Makete pamoja na wanaotoka katika vijiji vinavyounda kata ya Kipengere wilaya ya wanging'ombe walisema kilichokuwa kinasumbua miaka yote ni mkanganyiko kwenye ramani.

‘’Kwenye ramani kinasoma kingine,kwenye gazeti la serikali kinasoma kingine,mkienda kwenye ardhi mnaonyeshwa mahali pengine ,’’alisema Ebrania Mbilinyi.

Katibu Tawala mkoa wa Njombe Bi.Judica Omari alisema serikali imetoa fedha nyingi ili kufanikisha zoezi la upimaji wa ardhi.

Waziri pia alifika kusikiliza mgogoro wa Kanisa la Kiinjili la Kiluteri Tanzania Dayosisi ya Kusini na wakazi wa mtaa wa Lunyanywi na Magoda ambapo aliiagiza timu ya wataalamu kutoka wizara ya ardhi kufika na kufanya kazi ili kubaini ukweli.

‘’Na timu ikija itaongea na kila mtu mmoja mmoja,pia naagiza ujenzi usimame kwa sababu ni eneo la mgogoro mtu uwa anajenga sehemu yake,na sehemu hii kanisa linasema ya kwake na nyie mnasema ya kwenu,naahidi kurudi tena januari 2024 ili kumaliza mgogoro huu’’alisema Silaa.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASILI MKOANI NJOMBE KWA SHANGWE.

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA MTAKA AWAPONGEZA NA KUWAPA HAMASA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA MKOANI NJOMBE.

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA YA UONGOZI YA TASAF AMEANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI NJOMBE.

    April 28, 2025
  • HERI YA SIKU YA MUUNGANO.

    April 26, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.