• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

WADAU WA PARACHICHI WAFANYA MKUTANO WAO MKOANI NJOMBE

Posted on: January 10th, 2024

ASASI ya kilele inayoshughulisha na kilimo cha mbogamboga, matunda na mimea itokanayo na mizizi na viungo Tanzania Horticultural Association (TAHA) wamekabidhi vyeti vya hithibati kwa wakulima wapatao 300 wa Parachichi waliokidhi viwango vya kimataifa kufikia soko Barani Ulaya.

Hayo   yamelezwa na Mratibu wa Maendeleo Biashara kutoka TAHA, Asia Barnabas mara baada ya Mkutano wa jukwaa la wadau wa Parachichi uliofanyika mkoani hapa.

Barnabas alisema malengo ni kuhakikisha parachichi inayolimwa Tanzania inafikia masoko makubwa duniani.

“Na ili parachichi iweze kufikia masoko inatakiwa ianze kuwa na ubora kuanzia inapozalishwa, lakini tunaiomba sasa serikali yetu ya mkoa na serikali kuu kuhakikisha hizi changamoto ya kimiundombinu zinazosababisha parachichi hii pendwa isifikie mlaji au isifikie soko ziangaliwe,” alisema Barnabas.

Hata hivyo Barnabas amesema hakuna namna ya kufikia soko la dunia bila ya kuhakikisha kwamba changamoto zenye uzito mkubwa kwa wakulima na wafanyabiashara zinatatuliwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Anthony Mtaka aliwaagiza Wakala wa barabara Mjini na Vijijini (TARURA), Shirika la umeme (TANESCO) na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kuhakikisha kila taasisi inatatua changamoto katika eneo lake.

“Muanze mara moja mpango wa kujenga barabara zinazoelekea maeneo ya uwekezaji mkubwa, pia mnatakiwa kusogeza huduma ya umeme ili utumike kwa umwagiliaji mashambani na ushimbaji wa visima virefu kwa mkulima mmoja mmoja,” alisema Mtaka.

Mtaka amesema kuwa kabla ya kufikia hatua za kuchukua ushuru kwa wakulima ni vyema sasa huduma hizo zikaboreshwa ili wakulima waweze kuzalisha kwa tija na ubora unaotakiwa katika soko la dunia.

Mmoja wa wakulima hao, akiwemo Edger Mtitu alisema endapo mkakati wa kilimo na masoko uliyowekwa na serikali utafuatwa utaleta mageuzi katika uzalishaji pamoja na uchumi.

Pia ameomba serikali kudhibiti makampuni ambayo yananunua mazao ikiwemo parachichi Mkoa wa Njombe na kuyagonga nembo za Mataifa mengine hali ambayo inasababisha kuondoa uhalisia wa zao husika.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • KATIBU TAWALA MKOA WA NJOMBE APOKEA MADAKTARI BINGWA 37 KWA AJILI YA HUDUMA ZA AFYA.

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI.

    May 23, 2025
  • KATIBU TAWALA WA MKOA WA NJOMBE AWAKARIBISHA RASMI WAWEKEZAJI WA KIWANDA CHA PARACHICHI NJOMBE.

    May 22, 2025
  • MKUU WA MKOA NJOMBE ATOA UHAKIKA WA USHIRIKIANO KWA WAWEKEZAJI WA KIWANDA CHA PARACHICHI.

    May 22, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.