• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

VIJANA WA MKOA WA NJOMBE WAHAMASISHWA KUCHANGAMKIA FURSA YA MIKOPO YA KILIMO KWA MASHARTI NAFUU NA MKURUGENZI MTENDAJI WA MFUKO WA PEMBEJEO – [AGITF]

Posted on: September 25th, 2024


Na. Chrispin Kalinga - Njombe

Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Pembejeo, Bi Mwanahiba Mzee, ametoa wito kwa vijana wa Mkoa wa Njombe kuchangamkia fursa za mikopo ya kilimo inayotolewa na Taasisi hiyo, akisisitiza kuwa kilimo ni sekta yenye uwezo wa kuinua uchumi wa vijana na jamii kwa ujumla. Mkurugenzi alitoa rai hiyo wakati wa kikao kilichohudhuriwa na vijana na Wanawake wa Wilaya ya Njombe, kikao ambacho kiliendeshwa chini ya uongozi wa Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Mhe. Kissa Gwakisa.

Akizungumza na washiriki wa kikao hicho, Bi. Mwanahiba alieleza kuwa mikopo hiyo inalenga kuwasaidia vijana na Wanawake kuanzisha na kuendeleza miradi ya kilimo, ikiwa ni moja ya juhudi za Taasisi hiyo chini ya Wizara ya Kilimo katika kuimarisha sekta ya kilimo kwa vijana na wanawake  katika kupambana na tatizo la ukosefu wa ajira.

"Tunaamini kuwa kilimo kina uwezo mkubwa wa kubadilisha maisha ya vijana na Wanawake, na fursa za mikopo hii ni njia mojawapo ya kuwawezesha kufikia mafanikio. Nawahimiza vijana na Wanawake wote wa mkoa wa Njombe kuchangamkia fursa hii ili waweze kujijenga kiuchumi kupitia kilimo," alisema Mkurugenzi.

Aliongeza kuwa vijana wanahitaji kubadili mtazamo wao juu ya kilimo, akibainisha kuwa sekta hii sasa inahitaji ubunifu na teknolojia mpya ili kuongeza uzalishaji na tija.

"Kilimo siyo kazi ya kizamani; sasa hivi tunalenga kilimo cha kisasa kinachotumia teknolojia bora. Vijana wana nafasi kubwa ya kuleta mapinduzi ya kilimo hapa Njombe," alieleza Mkurugenzi.

Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Mhe. Kissa Gwakisa, aliunga mkono kauli hiyo na kuwaomba vijana kuchukua hatua za haraka katika kutumia mikopo hiyo ili waweze kujikwamua kiuchumi. Aliwahakikishia kuwa serikali inawaunga mkono kwa kuhakikisha mazingira bora ya kilimo yanakuwepo, pamoja na kuweka mipango ya kuwawezesha wakulima wadogo wadogo.

"Mikopo hii ni fursa nzuri kwenu vijana. Tunawaomba muwe mstari wa mbele kutumia nafasi hii kwa maendeleo yenu na ya jamii nzima. Ni wakati wa kuchukua hatua na kujenga maisha bora kupitia kilimo," alihimiza Mhe. Gwakisa.

Kikao hiki kilipata mwitikio mzuri kutoka kwa vijana, wengi wakionesha nia ya kujiunga na mpango wa mikopo ili kuanza safari ya kujiajiri kupitia kilimo.

Mfuko wa Pembejeo ni Taasisi iliyo chini ya Wizara ya Kilimo inayolenga kuondoa changamoto kwa wakulima wadogo kupata pembejeo za kilimo kwa gharama na masharti nafuu. Mfuko wa Pembejeo unatoa mikopo ya kilimo kwa riba ya asilimia 4.5 kwa ajili ya vijana na Wanawake, na riba ya asilimia 6 hadi 7 kwa wanaume waliozidi miaka 40.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MKUU WA MKOA WA NJOMBE MHE. ANTHONY MTAKA ASHIRIKI IBADA YA KUAGA MWILI WA MZEE MONGELLA JIJINI DAR ES SALAAM.

    June 04, 2025
  • KATIBU TAWALA NJOMBE AONGOZA KIKAO CHA MAANDALIZI YA MAONESHO YA NANENANE.

    June 04, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA NJOMBE APOKEA MADAKTARI BINGWA 37 KWA AJILI YA HUDUMA ZA AFYA.

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI.

    May 23, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.