• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

NAIBU WAZIRI TAMISEMI AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI NJOMBE

Posted on: October 9th, 2023

Naibu Waziri Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Mh. Deogratias Ndejembi,amegiza kufanyika kwa ujenzi usiku na mchana kwenye shule ya sekondari mpya inayojengwa kijiji cha Mbugani kata ya Kitandililo halmashauri ya Mji makambako mkoani Njombe yenye thamani ya zaidi ya  sh.milioni 500 kupitia mradi wa SEQUIP.

Ndejembi alilitoa agizo hilo jana mara baada ya kutembelea ujenzi huo na kubaini kususua ambapo alisema mafundi wanapaswa kuongezwa ili majengo hayo yakamilike kwa muda unaotakiwa.

"Nchi nzima mwisho ni tarehe 31 mwezi wa 10 mwaka huu sitabadilisha,hawa mafundi wamebana hela hawaweki nguvu ya kutosha ya kufanya kazi,tuko nyuma na deadline na iko palepale ya tarehe 31,nitarudi hapa tena bila ya hodi kuja kuona ujenzi unaendeleaje na hatua kubwa imefikiwa kumebadilika"alisema Ndejembi.

Aliongeza kuwa"kiukweli tunaenda taratibu tunamuangusha Rais wetu,tunamuangusha mbunge wetu ambaye tena yeye ndio mshika ilani ambayo haya yote yanayofanywa ni katika ilani ya uchaguzi ya chama cha mapinduzi,hapa hata choo hakijaanza kujengwa hivi tunavyozungumza na fundi mwenyewe site hayupo aliyepewa choo"alisema Ndejembi.

Naibu katibu mkuu ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Elimu)Dk Charles Msonde,aliahidi kufuatilia maendelea ya ujenzi wa shule hizo mpya nchi nzima ili kuhakikisha octoba 31 mwaka huu,shule zote za SEQUIP ziwe zimekwisha.

"Maelekezo haya umeshatoa tukiwa Dodoma hapa unayasisitiza tu na ndio maana umesita kuongeza hata siku moja na ni maelekezo najua ya mh waziri wa nchi,kwa hiyo wenzangu mafundi waongezwe kazi za sambamba usiku na mchana ili shule hizi zikamilike watoto wasiende kusoma umbali mrefu"alisema Msonde.

Awali mbunge wa jimbo la Makambako ambaye pia ni mwenyekiti wa chama cha mapinduzi CCM mkoa wa Njombe Deo Sanga,na Diwani wa kata ya Kitandililo Iman Fute walikiri mapungufu na walimuomba naibu waziri kuwaongezea muda.

"Naomba tuwe wakweli kabisa nikuombe kwamba kwamba tutakamilisha ifikapo tarehe 31 mwezi wa 10 tusikudanganye lakini nikuahidi kwamba haitavuka tarehe 20 ya mwezi wa 11 mambo yatakua yamekamilika kabisa,tuombe hizo wiki tatu za extension kwa maana ya kwamba tutapiga kazi kwa kushirikia na usiku na mchana tuhakikishe mambo yanakaa vizuri kama mlivyotukuta mh naibu waziri hatutoki"alisema Fute.

Akisoma taarifa mkuu wa shule ya sekondari Kitandililo Albert Kahonga,alisema serikali imetoa kiasi cha zaidi ya sh.milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ili kuwaondolea wanafunzi changamoto ya kutembea umbali mrefu.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MKUU WA MKOA WA NJOMBE MHE. ANTHONY MTAKA ASHIRIKI IBADA YA KUAGA MWILI WA MZEE MONGELLA JIJINI DAR ES SALAAM.

    June 04, 2025
  • KATIBU TAWALA NJOMBE AONGOZA KIKAO CHA MAANDALIZI YA MAONESHO YA NANENANE.

    June 04, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA NJOMBE APOKEA MADAKTARI BINGWA 37 KWA AJILI YA HUDUMA ZA AFYA.

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI.

    May 23, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.