• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

KIWANDA CHA KUCHAKATA PARACHICHI NJOMBE CHAJA NA FURSA ZAIDI YA AJIRA 1,500 KWA VIJANA IFIKAPO MACHI 2025

Posted on: December 13th, 2024

Njombe, Desemba 13, 2024 – Uongozi wa Kampuni ya Avocado Avenue Tanzania Ltd ukiongozwa na Bw. Amin Manji, leo umefika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe na kupokewa rasmi na Mkuu wa Mkoa, Mhe. Anthony Mtaka.

Katika mazungumzo yao, walijadili masuala muhimu yanayolenga kuimarisha uchumi wa wakulima wa parachichi mkoani Njombe. Miongoni mwa mambo yaliyopatiwa msisitizo ni kuanza kwa ujenzi wa kiwanda cha kuchakata parachichi ambacho pia kitatengeneza mafuta ya parachichi. Aidha, kampuni hiyo imeahidi kununua parachichi zote, ikiwemo zile zilizokataliwa, na kuzigeuza kuwa bidhaa mbalimbali kwa ajili ya masoko ya ndani na ya kimataifa.

Mbali na kiwanda, Avocado Avenue Tanzania Ltd imeeleza mipango yao ya kutoa soko endelevu la parachichi kwa wakulima wa Njombe. Kampuni hiyo pia imeahidi kutekeleza programu za kuwawezesha wakulima kwa:
✅ Kutoa maarifa ya kitaalamu kuhusu kilimo bora cha parachichi.
✅ Kutoa msaada wa utunzaji wa mazao.
✅ Kuwasaidia wakulima kufanikisha mavuno bora na kuendeleza kilimo endelevu.

Kiwanda hicho kinatarajiwa kukamilika mwezi Machi 2025, ambapo kampuni hiyo itaanza kupokea mazao ya parachichi kutoka kwa wakulima. Aidha, kiwanda hicho kitatoa ajira za kudumu kwa watu 100 na ajira za mikataba kwa takriban watu 300, huku wakitarajia kushirikiana na kuwafikia zaidi ya wakulima 1,500.

Mhe. Anthony Mtaka ameipongeza Avocado Avenue Tanzania Ltd kwa kuamua kuwekeza mkoani Njombe. Akizungumza wakati wa kikao hicho, alisema:
“Nawashukuru sana kwa kuja kuwekeza katika sekta ya parachichi mkoani Njombe. Uamuzi wa kujenga kiwanda cha kuchakata parachichi hapa Njombe utaongeza thamani ya tunda hili moja kwa moja kuanzia hapa hapa mkoani. Hatua hii itakuza uchumi wa wakulima wetu na kuongeza ajira kwa wananchi wa Njombe na maeneo ya jirani.”

Kampuni ya Avocado Avenue Tanzania Ltd imeonyesha dhamira ya dhati ya kushirikiana na mkoa wa Njombe kuimarisha sekta ya kilimo cha parachichi na kuboresha maisha ya wakulima.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MKUU WA MKOA WA NJOMBE MHE. ANTHONY MTAKA ASHIRIKI IBADA YA KUAGA MWILI WA MZEE MONGELLA JIJINI DAR ES SALAAM.

    June 04, 2025
  • KATIBU TAWALA NJOMBE AONGOZA KIKAO CHA MAANDALIZI YA MAONESHO YA NANENANE.

    June 04, 2025
  • KATIBU TAWALA MKOA WA NJOMBE APOKEA MADAKTARI BINGWA 37 KWA AJILI YA HUDUMA ZA AFYA.

    May 26, 2025
  • MCHENGERWA: MAAFISA HABARI HAKIKISHENI WANANCHI WANAPATA HABARI SAHIHI.

    May 23, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.