• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

UMEME WA ACRA-LUGARAWA WA MEGAWATI 1.7 KUNUFAISHA KATIKA UCHUMI WA VIWANDA WANANCHI WA VIJIJI ISHIRINI WILAYA YA LUDEWA MKOANI NJOMBE

Posted on: September 21st, 2019

UMEME WA ACRA-LUGARAWA MEGAWATI 1.7 KUNUFAISHA WANANCHI WA VIJIJI ISHIRINI KATIKA UCHUMI WA VIWANDA WILAYA YA LUDEWA MKOANI NJOMBE

WANANCHI wa Kata ya Lugarawa, Wilayani Ludewa Mkoani Njombe wameipongeza serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk. John Magufuli kwa hatua ya kuwaletea umeme wa maji unaofadhiliwa na shirika la ACRA utakaowezesha upatikanaji wa umeme wa kilowati 1700 ambao ni sawa megawati 1.7.

Kati ya umeme huo, megawati 0.7 zitatumiwa na kata sita zilizopo kwenye wilaya ya Ludewa na kuhudumia wananchi wanaoishi katika vijiji 20.

Hayo yamesemwa na msoma risala wa mradi huo ambae ni Afisa maendeleo ya jamii wa kata ya lugarawa Oresta Mkalawa wakati mbio za mwenge wa uhuru zilipokwenda kuweka jiwe la msingi katika mradi huo wa umeme unaozalisha nishati ya umeme kwa kutegwa kwa bwawa kubwa lililopo juu yam lima kutokana na vyanzo mbalimbali vya maji ya chemichem vinavyopatikana kwenye kata hiyo.

Mradi huo ulioanza kujengwa tangu mwaka 2014 chini ya usimamizi wa shirika la ACRA ikishirikiana na kanisa Katoliki Jimbo la Njombe na kampuni ya Studio Frosio ya nchini Italia utazinduliwa mwezi Oktoba mwaka huu ukiwa umegharimu zaidi ya shilingi bilioni 19.8.

Baadhi ya wananchi waliozungumzia mradi huo akiwemo Bosco Mgimba ambaye ni mkazi wa kata ya Lugarawa amesema “wanashukuru sana kwa mradi huu utatunufaisha katika mambo mengi kama vile kwa kuwa mwanzoni matumizi tuliyokuwa tukiyatumia ndani ya nyumba ni kuwasha mishumaa ndani ya nyumba, vibatali na hata kutumia mafuta ya taa, lakini kwa ujio wa mradi huu tutaweza kuanzisha viwanda vyetu vidogo,” amesema Bosco Mgimba.

Oresta Mkalawa ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii wa Kata ya Lugarawa amesema jumla ya wajisiamali wadogo na wakati 340 watanufaika katika mradi huo na kati yao 40 watasaidiwa na shirika la ACRA kwa  kununuliwa vifaa vya kuanzisha viwanda pamoja na mafunzo.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Ludewa, Andrea Tsere amesema wilaya ya Ludewa wapo wananchi wenye ujuzi na maarifa wakutaka kusukuma gurudumu la maendeleo ya kiuchumi ili kuitikia rai ya serikali ya kuwa na Tanzania ya Viwanda, lakini kwa kipindi kirefu kikwazo cha kufikia lengo lao kwenye maeneo ya vijijini ilikuwa ni kukosekana kwa nishati ya umeme ambayo ingekuwa msaada wa kuanzisha viwanda vidogo na vya kati.

Mradi huo wa umeme wa maji uliopitiwa na Mwenge wa Uhuru na kuwekwa jiwe la msingi baada ya kupongezwa na kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa, Mzee Mkongea Ali,ambapo amesema ni vyema wananchi wakaichangamkia fursa ya upatakinaji wa nishati hiyo ya umeme ili kuweza kubadilisha maisha yao kiuchumi.


Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASILI MKOANI NJOMBE KWA SHANGWE.

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA MTAKA AWAPONGEZA NA KUWAPA HAMASA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA MKOANI NJOMBE.

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA YA UONGOZI YA TASAF AMEANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI NJOMBE.

    April 28, 2025
  • HERI YA SIKU YA MUUNGANO.

    April 26, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.