• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

SERIKALI YAENDELEA NA MAZUNGUMZO NA MWEKEZAJI WA MRADI LIGANGA NA MCHUCHUMA

Posted on: January 6th, 2024

Serikali imesema iko mbioni kukamilisha mazungumzo na mwekezaji wa mradi wa Liganga na Mchuchuma uliopo Wilayani Ludewa Mkoa wa Njombe kwa kuzingatia sheria ya mapitio na majadiliano kuhusu mkataba yenye masharti hasi.

Waziri wa Katiba na Sheria, Balozi Dkt. Pindi Chana ameyasema hayo wakati alipotembelea eneo la mradi huo, amesema mazungumzo hayo yanakwenda sambamba na kuhakikisha rasilimali za nchi zinatumika kuongeza pato la taifa na kuleta maendeleo.

“Sasa ni dhamira ya dhati kabisa ya kusema kwamba mradi unakwenda kuanza tunayo malengo kwenye Ilani yetu ya chama ya mapinduzi lakini pia katika maono yetu ya 2025 tumeeleza wazi huu ni mradi muhimu,” alisema Dk. Chana.

Waziri Dkt. Chana alisema kuwa watanzania wanayo kiu ya kuona kwamba mradi huo wa kimkakati wa liganga na mchuchuma unaanza mara moja.

“Sisi kama wizara ya katiba na sheria kwa kushirikiana na wizara ya viwanda na Biashara waziri mwenzangu anayesimamia masuala la viwanda tunaendelea kusimamia suala hili kwa karibu sana,” alisema waziri Dk. Chana.

Pia Dkt. Chana alibainisha kwamba, “Na tunataka miradi hii ya mchuchuma na liganga iwanufaishe watanzania wote kama jinsi ambavyo sheria zetu tulizopitisha mwaka 2017 zinavyosema mali asili za taifa, mali asilia zinapaswa kutumika kwa manufaa na faida ya watanzania wote,” alisema.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Uangalizi na Utajiri wa Rasilimali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Neema Mwanga alisema mchakato wa mradi huo upo kwenye mazungumzo ili kupitia sheria za mikataba.

“Mnamo mwaka 2017 Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania lilitunga sheria mbili, sheria ya mamlaka ya nchi kuhusu umiliki wa utajiri na maliasili za nchi na sheria ya mapitio na majadiliano kuhusu mikataba yenye masharti hasi,” alisema Mwanga.

Mwanga anafafanua kuwa, “Sheria hii ya pili inataka mikataba yote inayoingiwa na wawekezaji katika uchimbaji au uvunaji na matumizi ya utajiri na mali asili za nchi ulenge katika kuhakikisha rasilimali zinapatikana, kuongeza pato la taifa lakini kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi,” alisema.

Aidha alisema kuwa kwa sababu nchi inahitaji wawekezaji, hivyo ni lazima mikataba inayoingiwa iwe na tija kwa sababu sheria zimesisitiza.

Meneja Mradi wa Liganga na Mchuchuma kutoka Shirika la Taifa la Mendeleo (NDC) Dk. Witness Ishuza alisema kwa mujibu wa tafiti zilizofanyika katika eneo la liganga kuna tani zaidi ya milioni 128 za chuma.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASILI MKOANI NJOMBE KWA SHANGWE.

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA MTAKA AWAPONGEZA NA KUWAPA HAMASA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA MKOANI NJOMBE.

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA YA UONGOZI YA TASAF AMEANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI NJOMBE.

    April 28, 2025
  • HERI YA SIKU YA MUUNGANO.

    April 26, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.