• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

MKUU WA MKOA WA NJOMBE AENDELEA NA ZIARA KATIKA KITUO CHA AFYA NJOMBE MJINI

Posted on: November 27th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mh. Anthony Mtaka amemuagiza Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Njombe Bi Kuruthum Sadick kuwasimamisha kazi watumishi sita wa kituo cha afya cha mjini hapo baada ya kubainika upotevu wa vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya sh.milioni 15.

Agizo hilo lilitolewa  wakati wa ziara ya mwendelezo ya Kamati ya Ulinzi na Usalama   ya Mkoa  kushughulikia matukio ya wizi yanayotokea katika hospitali na vituo vya afya mkoani hapa.

“Mkurugenzi uchukue hatua hapa simamisha na hatua za haraka za kinidhamu zifanyike kwa kufuata taratibu zote na Mkuu wa kituo cha Polisi tukitoka hapa beba hawa watu wote nenda nao wakatoe maelezo,wakitoa maelezo hatua za kinidhamu za kiutumishi na uchunguzi ufanyike,”alisema Mtaka.

Awali akisoma taarifa ya upotevu, Mganga Mkuu Halmashauri ya Mji Njombe Dk. Jabil Juma alisema vifaa tiba vilivyoibiwa ni kipimo cha wingi wa damu,mashine ya kupima mkojo,vitepe kwa ajili ya kupima Ukimwi.

“Mshine moja ya uchunguzi wa mkojo haikuonekana stoo ilipokelewa Januari 2022, lakini pia tulibaini mashine moja ya uchunguzi wa wingi wa damu pia haikuwepo maabara,”alisema Juma.

Watuhumiwa wa upotevu huo akiwemo aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Maabara,Izack Kayombo alisema mashine ya kupima wingi wa damu waliiazimisha katika kituo cha afya Lupembe halmashauri ya wilaya ya Njombe.

Hata hivyo Mganga Mkuu wa Mkoa wa Njombe,Dk.Juma Mfanga alisema katika ufuatiliaji wake taarifa hizo vifaa hivyo havipo maeneo yanapoelezwa vimepelekwa.

“Kwenye ufuatiliaji ambao tumeufanya imeonekana kwamba mashine ya kupima mkojo ndio ilienda kituo cha afya Lupembe kwa sababu tunasimamia vituo vyote vya afya kwenye mkoa wao wanakiri hawajapokea,inamaana kuna mahali hapa katikati viliishia,”alisema Mfanga.

Wakati huo huo,Mkuu wa Mkoa alisema inasikitisha kuona kwamba inafika mahala unakuwa na watumishi ambao unawaajiri alafu wanaiba.

‘’Kwanza nikuombe Mganga Mkuu wa Mkoa kufanyike ukaguzi vituo vyote vya afya vya mkoa wa Njombe,ukaguzi ufanyike hospitali zote za wilaya mkoa wa Njombe tuangalie vifaa tulivyopokea,utokaji wake,vilivyopo na ambavyo vimetumika hiyo taarifa tuwe nayo kwa sababu tusije tukawa na vifaa alafu tuna madalali kwenye ofisi za umma,’’alisema Mtaka.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe,Kamishna msaidizi Mahmoud Banga alisema hadi sasa watu 10 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa ajili ya uchunguzi wa tuhuma za wizi katika kituo cha afya Njombe mjini na hospitali ya rufaa mkoa wa Njombe.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • PROF. MUKANDALA AONGOZA VIONGOZI KUSHUHUDIA UTIAJI SAINI WA MKATABA WA UJENZI WA KAMPASI YA UDOM MKOANI NJOMBE.

    May 17, 2025
  • MPANGO WA NJOMBE KUPUNGUZA UDUMAVU WAZINDULIWA RASMI.

    May 17, 2025
  • KAMATI YA USALAMA YA MKOA WA NJOMBE YAMPA POLE KAMISHNA MWANDAMIZI WA UHAMIAJI FELISTA SANGA KUFUATIA MSIBA WA MUMEWE.

    May 17, 2025
  • MKUU WA MKOA WA NJOMBE MHE. ANTHONY MTAKA AKUTANA NA MKURUGENZI WA KAMPUNI YA KANJI LALJI, AMKARIBISHA KUWEKEZA MKOANI NJOMBE KATIKA KILIMO CHA KAHAWA.

    May 17, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.