• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI YAKAGUA MRADI WA UMEME MAKETE, YATOA PONGEZI KWA REA.

Posted on: March 17th, 2025

Makete, 17 Machi 2025

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Dkt. David Mathayo David, pamoja na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga, na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), leo imeendelea na ziara yake mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini wilayani Makete. Katika ziara hiyo, Kamati ilitembelea kijiji cha Mang’oto na kutoa pongezi kwa REA kwa kusimamia mradi huo kwa ufanisi na kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme.

Akizungumza baada ya ukaguzi wa mradi huo, Mwenyekiti wa Kamati, Mhe. Dkt. David Mathayo David, aliipongeza REA kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kusambaza umeme vijijini. Aidha, aliutaka mkandarasi kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi ili maeneo yote yaliyopangwa yaunganishwe kwa wakati. "Tunawapongeza REA kwa kazi nzuri ya kusimamia miradi ya umeme vijijini, hususan hapa Mang’oto. Hata hivyo, tunamtaka mkandarasi kuongeza kasi ili kuhakikisha wananchi wote wanafaidika na huduma hii muhimu," alisema Dkt. Mathayo.


Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga, aliwahakikishia wananchi kuwa serikali inaendelea kutatua changamoto zote za umeme nchini na kuhakikisha vitongoji vyote vinapata nishati ya umeme ili kuboresha huduma za kijamii na kukuza uchumi wa wananchi. "Serikali imejipanga kuhakikisha kila kijiji na kitongoji kinapata huduma ya umeme. Lengo letu ni kuimarisha huduma za afya, elimu na kuwezesha biashara kufanyika usiku na mchana bila vikwazo," alisema Mhe. Kapinga.


Mkurugenzi wa REA, Mhandisi Jones Olotu, alisema serikali inaendelea kuongeza kasi ya usambazaji wa umeme vijijini, ambapo hivi karibuni wanatarajia kutangaza tenda nyingine ili kuongeza nguvu katika utekelezaji wa miradi hiyo. "Tunatambua kuwa umeme ni kichocheo muhimu cha maendeleo. Kwa kutambua hilo, tutaongeza juhudi kuhakikisha maeneo yote yaliyobaki yanafikiwa kwa wakati," alisema Mhandisi Olotu.


Wananchi wa Mang’oto wameeleza furaha yao kwa kupata huduma ya umeme kupitia mradi wa REA, wakisema kuwa nishati hiyo imeleta mabadiliko makubwa katika shughuli za uzalishaji na biashara. Mkazi wa kijiji hicho, Bw. Daniel Mbilinyi, alituma salamu za shukrani kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuwekeza katika miradi inayowanufaisha wananchi wa vijijini. Katika ziara hiyo, Kamati ya Bunge pia ilifanya mkutano wa hadhara na wananchi wa eneo hilo, ambapo walipata fursa ya kutoa maoni yao kuhusu miradi ya umeme na maendeleo kwa ujumla.



Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASILI MKOANI NJOMBE KWA SHANGWE.

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA MTAKA AWAPONGEZA NA KUWAPA HAMASA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA MKOANI NJOMBE.

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA YA UONGOZI YA TASAF AMEANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI NJOMBE.

    April 28, 2025
  • HERI YA SIKU YA MUUNGANO.

    April 26, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.