• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

IDADI YA WATALII YAONGEZEKA TANZANIA

Posted on: September 26th, 2022

Waziri wa maliasili na utalii Mhe. Pindi Chana,amesema kwa kipindi cha mwezi januari hadi julai mwaka huu jumla ya watalii zaidi ya 4000 walikuja nchini ikilinganishwa na watalii kwa kipindi cha januari hadi julai 2021.

Hatua hiyo imeelezwa  jana na waziri huyo wakati wa uzinduzi wa mkakati wa kutangaza utalii kusini mwa Tanzania uliofanyika mkoani Njombe ambapo alisema ni mafanikio ya mpango wa Royar Tour na kwamba watalii wanaendelea kumiminika.

Akizungumzia changamoto alisema licha ya sekta ya utalii kuwa na mchango mkubwa katika uchumi wa nchi lakini mchango huo hauakisi utajiri wa rasilimali za utalii zilizopo hapa nchini.

Pindi alisema changamoto nyingine inatokana na watalii wengi wanaokuja nchini kutembelea zaidi vivutio vya utalii vilivyopo ukanda wa kaskazini ikiwemo hifadhi za taifa za Kilimanjaro, Serengeti, Ziwa Manyara na eneo la hifadhi ya Ngorongoro.

Alisema hali hiyo inasababisha siku za watalii  ambao wanakuja hapa nchini kukaa kuendelea kuwa chache na watalii kutojirudia.


Alisema katika kufungua utalii kwenye vivutio vya nchi mwaka 2017 serikali ilianzisha mradi wa kuboresha usimamizi wa maliasili na kukuza utalii kusini mwa Tanzania kwa lengo la kupanua wigo wa mazao ya utalii kijiografia kwa kuendeleza sekta hiyo katika mikoa ya kusini.

"Mradi huo unatekelezwa kupitia fedha za mkopo wa masharti nafuu wa dola za Marekani milioni 150 kutoka benki ya dunia" alisema Dk. Chana.


Alisema katika kufanikisha azma ya kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo mikoa ya kusini wizara ya maliasili na utalii kupitia bodi ya utalii Tanzania imeendaa mikakati mahususi ya kutangaza vivutio vya utalii.

Kaimu mkurugenzi wa bodi ya utalii Tanzania Felix John,alisema utalii ni moja ya sekta za vipaumbele hapa nchini na Rais Samia Suluhu Hassan amejitoa kupitia programu maalum ya Tanzania Royal Tour ili kuitangaza na kuifungua nchi katika sekta ya utalii.

John alisema bodi hiyo imejipanga ili kufungua utalii wa nyanda za juu kusini kwa kuleta watalii kwenye vivutio vilivyopo katika mikoa hiyo.

"Kama mnavyofahamu vipo vivutio vingi katika ukanda huu wa kusini tunayo Kitulo, Mpanga Kipengele na eneo la kihistoria la nyumbanitu" alisema John.

Mkuu wa mkoa wa Njombe Anthony Mtaka alisema Tanzania ina hifadhi nyingi na zinafanana lakini upekee uliopo kwa mkoa wa Njombe ni hifadhi ya Kitulo ambayo ni maalum kwa uhifadhi wa maua.

"Kwa maana kama shughuli inafanyika Dar es salaam haya maua inabidi waagize kutoka sehemu nyingine lakini kama ni Njombe yanapatikana hapa hapa" alisema Mtaka.

Alisema watu wengi hawafahamu kuwa hata biashara ya maua inayofanyika mkoa wa Kilimanjaro wilaya ya Moshi na Arusha ilianzia mkoani Njombe.

Alisema biashara hiyo haikufanyika mkoani Njombe kutokana na kukosekana kwa miundo mbinu ya  uwanja wa ndege.

Baadhi ya wabunge wa mkoa wa Njombe wakiwemo Joseph Kamonga na Deo Sanga walisema ili utalii ulete tija kwenye mkoa wa Njombe waliiomba serikali kuharakisha ujenzi wa uwanja wa ndege kwasababu utalii unakwenda sambamba na usafiri wa uhakika.

"Uwanja wetu wa ndege hapa ukamilike ili watalii wawe wanashuka na kuja kwa njia ya ndege na mambo mengine kama kusafirisha parachichi zetu" alisema Sanga.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • MWENGE WA UHURU 2025 WAWASILI MKOANI NJOMBE KWA SHANGWE.

    May 03, 2025
  • MKUU WA MKOA MTAKA AWAPONGEZA NA KUWAPA HAMASA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA MKOANI NJOMBE.

    April 29, 2025
  • MWENYEKITI WA KAMATI YA TAIFA YA UONGOZI YA TASAF AMEANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI NJOMBE.

    April 28, 2025
  • HERI YA SIKU YA MUUNGANO.

    April 26, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.