• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

ATOA HUDUMA ZA AFYA WATAKIWA KUTOWASAHAU WATOTO KATIKA KUWAKINGA NA MAAMBUKIZI YA VVU

Posted on: October 6th, 2018

Serikali kupitia Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na watoto imewataka watoa huduma za afya nchini kutokuwasahau watoto na vijana katika kuwakinga na maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU).

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa uzinduzi wa Mkakati wa wauguzi na wakunga kusogeza huduma za VVU na UKIMWI karibu na jamii ikiwemo ushauri nasaha, kupima VVU na kufuatilia maendeleo ya afya za walengwa uliofanyika mapema leo mkoani Njombe.

“Bado tuna changamoto kwa watoa huduma wetu wa afya kwa baadhi ya maeneo ikiwemo kutokuwapima watoto hali ya maambukizi, kutoa dawa kwa watoto na kuwapa elimu vijana hivyo natoa rai kwa wahudumu wa afya tuweze kuweka mkakati wa kufikia makundi hayo” alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha Dkt. Ndugulile amewasisitiza Wauguzi na Wakunga kutoa huduma kwa kuzingatia miiko na maadili hususan katika kutoa huduma za VVU kwa jamii inayowazunguka ikiwemo kutumia lugha nzuri na kuwa wanyenyekevu kwa wananchi.

Sambamba na hilo Dkt. Ndugulile amewaasa wanaume nchini kuacha uoga na kujitokeza kupima VVU ili kutambua afya zao na kuanza matibabu mara moja iwapo watakutwa na maambukizi.

“Tutawafuata wanaume popote walipo hususan waliopo kwenye mikusanyiko yao ikiwemo kwenye sehemu za starehe, viwanja vya mipira , Migodini na sehemu za uvuvi ili kutoa elimu na kuwashauri wapime ili kujua afya zao” alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha Dkt. Ndugulile amesema kusudio la kufanya hivyo ni kuhakikisha kufikia malengo ya 90 90 90 ya kutokuwa na maambukizi mapya ifikapo mwaka 2030. Ambapo asilimia 90 ya watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi wawe wanajua hali zao za maambukizi.

Ili kutimiza malengo ya serikali katika kupambana na maambukizi, Dkt Ndugulile amesema Serikali imekuja na utaratibu wa dawa kinga ambapo dawa hizo zitatumika kwa makundi maalumu ambayo yako hatarini kupata maambukizi.

“Lakini vile vile tumekuja na utaratibu unaoitwa dawa-kinga ambazo kuna makundi ambayo tumebaini, ambayo yako kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi ya UKIMWI. Makundi haya kuna dawa ambayo tunataka tuwape zisaidiane na kinga nyingine ili kusaidia watu wasipate maambukizi ya virusi vya UKIMWI lakini hatusemi kwamba tumeshapata kinga”. Dkt Ndugulile.

Sambamba na hayo Dkt. Ndugulile amewataka watoa huduma waende wakatoe msisitizo na kuelimisha jamii katika maeneo ambayo dawa-kinga zimeanza kufanyiwa majaribio ili kuleta matokeo chanya.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Njombe Christopher Ole Sendeka amesema ukanda wa nyanda za juu kusini ni ukanda ambao una maambukizi makubwa ya VVU na serikali ya mkoa ilianza kampeni ya tohara kwa wanaume, na sasa inaelekea kwa watoto wa sekondari na shule ya msingi ikiwa ni njia mojawapo ya kupambana na maambukizi mapya.

“Takwimu zinaonesha sisi tuna kiwango kikubwa cha maambukizi kuliko katika ukanda ule ambao tohara kwa wanaume inaanzia katika umri mdogo kiwango cha maambukizi kiko chini lakini pia kuna mahusiano kati aya tohara ya wanaume na maambukizi ya VVU kwahiyo kama mkoa kampeni hii tumeivalia njuga chini ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na TAMISEMI”. Alisema Ole Sendeka.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na Waganga Wakuu wa mikoa na Wafawidhi wa mikoa mbalimbali pamoja na wauguzi na wakunga waliopata muongozo wa kusogeza huduma za VVU na UKIMWI karibu na jamii ikiwemo ushauri nasaha, kupima VVU na kufuatilia maendeleo ya afya za walengwa.

Christopher philemon

Afisa habari Mkoa wa Njombe

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • DR. MICHAEL HAULE WA NM-AIST AMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA NJOMBE.

    June 25, 2025
  • MWEKEZAJI NEIL GOODTILLERE WA BROWNS PLANTATION AKUTANA NA MKUU WA MKOA WA NJOMBE.

    June 25, 2025
  • MAFUNZO MAALUMU KWA MADEREVA WA TAASISI ZA SERIKALI YAENDELEA MKOANI NJOMBE.

    June 14, 2025
  • MKUU WA MKOA WA NJOMBE MHE. ANTHONY MTAKA ASHIRIKI IBADA YA KUAGA MWILI WA MZEE MONGELLA JIJINI DAR ES SALAAM.

    June 04, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.