• Complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
MKOA WA NJOMBE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government MKOA WA NJOMBE

  • Home
  • About Us
    • Historical Background
    • Mission and Vision
    • Core Values
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections
      • Administration & HR Section
      • Local Government Section
      • Planning & Coordination Section
      • Economic & Production Section
      • Infrastructure Section
      • Education Section
      • Health Section
    • Units
      • Finance & Accounts Unit
      • Internal Audit Unit
      • ICT Unit
      • Procurement & Supply Unit
      • Legal Unit
  • District
    • Njombe District
    • Wanging'ombe District
    • Makete District
    • Ludewa District
  • Councils
    • Njombe TC
    • Njombe DC
    • Wanging'ombe DC
    • Makete DC
    • Ludewa DC
    • Makambako Tc
  • Investment Opportunities
    • Agriculture
      • Crop production
      • Livestock
      • Fisheries
      • Forestry
    • Tourism
    • Mining
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • ICT Services
    • Infrastructure Services
    • Water Services
  • Publications
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Laws
    • Forms
    • Strategic plan
    • Client Service Charter
  • Media Center

Agricultural Services

Mkoa una eneo la kilomita za mraba 24,994 sawa na hekta 2,499,400 ambapo eneo linalofaa kwa kilimo ni hekta 1,090,000 sawa na asilimia 43.6. Katika eneo hilo eneo lililolimwa kwa msimu 2017/18 ni hekta 368,530 sawa na asilimia   34 ya eneo linalofaa kwa kilimo.

Mkoa umepata mafanikio ya sekta hii katika maeneo ya upatikanaji wa chakula, kuongeza uzalishaji wa mazao ya biashara, na upatikanaji wa mbolea.

Hali ya chakula kwa msimu wa 2018/ 2019

Kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2017/18, Mkoa umezalisha tani 602,362  za mazao ya nafaka na tani  766,003 za  viazi mviringo, viazi vitamu, ndizi na mhogo pamoja na tani 54,473  za mikunde  na kufanya jumla ya  tani 1,422,838.

Hivyo, kiasi halisi cha chakula kitakachopatikana kwa msimu wa 2018/19 kuwa tani 855,143 (Nafaka tani 602,362 na tani 252,781 ya viazi mviringo, viazi vitamu, ndizi na mhogo baada ya kuondoa maganda, na tani 54,473 za Mikunde).

Kwa mwaka, Mkoa unahitaji tani 173,621 za chakula ambapo chakula kilichopatikana (msimu 2017/18) ni tani 855,143, hivyo Mkoa ulikuwa na ziada ya tani 681,522 za chakula kama ilivyooneshwa kwenye kiambatisho Na. 2.

Uzalishaji wa mazao ya Biashara

Mazao ya biashara yanayolimwa ndani ya Mkoa ni pamoja na Chai, Pareto, Maua, Alizeti, Kahawa, Ufuta, Korosho, Miwa, Matunda ya aina mbali mbali, Shayiri na Karanga. Kwa mwaka 2017/18 tani 86,964 za mazao ya biashara zilivunwa kutoka eneo la ukubwa wa heka 37,471 kama inavyooneshwa kwenye jedwali Na. 37.

Jedwali Na. 37: Uzalishaji wa Mazao ya Biashara kwa msimu wa mwaka 2017/18

Na

Zao

Hekta zilizolimwa

Tani  zilizovunwa


Alizeti

13,216

12,243


Pareto

1,388

1,094


Kahawa

149

564


Chai

8149

42,071


Korosho

10

8


Matunda

8,385

21,270


Miwa

138

2,735


Maua

2

2


Ufuta

322

379


Karanga

5,142

6,597

 
Jumla

37,471

86,964

Uzalishaji wa Parachichi

Zao la Parachichi limeanza kupata umaarufu mkubwa kuanzia msimu wa 2016/2017 ambapo makampuni ya ndani na nje ya Nchi yalionesha nia ya kununua zao hilo. Katika msimu wa mwaka 2017/2018 jumla ya hekta 1,597 zilipandwa parachichi aidha, uzalishaji ulifikia tani 3,211 na kati ya hizo tani 38.3 zilinunuliwa na makampuni Makampuni ya Lima Kwanza Tanzania Ltd na Tanzanice yaliyosafirisha Parachichi hizo nchi za Ubelgiji, Uholanzi, na Uingereza. Makampuni mengine yaliyonunua parachichi ni pamoja na KUZA AFRICA COMPANY LTD, KEITT, Simba Logistic Equipment Supply. Wakulima waliuza kwa bei ya wastani kati ya shilingi 1000 hadi 1,500 kwa kilo moja.

Kampuni ya Alvardo imeanza maandalizi ya kujenga kiwanda cha kusindika parachichi katika halmashauri ya Wanging’ombe.

Kutokana na mafanikio haya makubwa (upatikanaji wa soko na Ujenzi wa kiwanda), Mkoa umejipanga kushirikiana nawadau mbalimbali kuendelea kutoa elimu kwa wakulima na jamii kwa ujumla ili kuwezesha uzalishaji wa parachichi za kutosha zenye ubora unaokidhi mahitaji ya soko.

Upatikanaji wa mbolea.

Mkoa una mbolea ya kutosha kwa matumizi ya wakulima kwa musimu wote wa kilimo. Bei elekezi ya Serikali inatumika kwa mbolea za DAP na UREA, hali hii imesaidia kutopanda kwa bei kiholela na kuwafanya wakulima wengi kumudu kuinunua.

Huduma za Ugani

  • Mkoa hivi sasa una jumla ya wataalam 263 wa Kilimo ukilinganisha na mahitaji ya watumishi 452 sawa na asilimia 58 hivyo kuwepo kwa upungufu wa maafisa ugani 189.

Announcements

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2024MKOA WA NJOMBE January 08, 2024
  • TAARIFA KWA UMMA May 10, 2023
  • TAARIFA YA UHAMISHO OFISI YA MKUU WA MKOA WA NJOMBE October 14, 2023
  • View All

Latest News

  • DR. MICHAEL HAULE WA NM-AIST AMTEMBELEA MKUU WA MKOA WA NJOMBE.

    June 25, 2025
  • MWEKEZAJI NEIL GOODTILLERE WA BROWNS PLANTATION AKUTANA NA MKUU WA MKOA WA NJOMBE.

    June 25, 2025
  • MAFUNZO MAALUMU KWA MADEREVA WA TAASISI ZA SERIKALI YAENDELEA MKOANI NJOMBE.

    June 14, 2025
  • MKUU WA MKOA WA NJOMBE MHE. ANTHONY MTAKA ASHIRIKI IBADA YA KUAGA MWILI WA MZEE MONGELLA JIJINI DAR ES SALAAM.

    June 04, 2025
  • View All

Video

Music
More Videos

Quick Links

  • Vivutio vya Utalii mkoani Njombe
  • Fursa za kilimo cha matunda aina ya maparachichi
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024/2025
  • Maktaba ya Picha
  • Maktaba ya Video

Related Links

  • Tovuti ya Temesa
  • Tovuti ya Tanroads
  • Tovuti ya Wizara ya Ujenzi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Contact Us

    Mtaa wa Lunyanywi

    Postal Address: P.O.Box 668-Njombe

    Telephone: 026 278 291 213

    Mobile:

    Email: ras@njombe.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2019 GWF . All rights reserved.